MUHADHARA WA TATU: VIPINDI VYA USHIRI WA KISWAHILI
MUDA SAA:
MHADHIRI; KADAWI
VIPINDI VYA USHAIRI.
Chimbuko la ushairi.
Ushairi kama utanzu wa fasihi, chimbuko lake linahusishwa na
chimbuko la fasihi na sanaa kwa ujumla, chimbuko la fasihi ukiwemo ushairi ni
kazi, na fasihi ya kwanza katika historia ya fasihi ni wimbo wa kazi. Wimbo ni
utanzu wa ushairi hivyo tunashawishika kusema kuwa fasihi ya kwanza ni ushairi
simulizi.
Ushairi unahusishwa na kazi kwa sababu chimbuko la kazi,
hivyo basi kazi ina dhima kubwa katika asili na chimbuko la fasihi ukiwemo
ushairi kama utanzu mkongwe kuliko mwingine.
Kwa vile fasihi ni sanaa inayotumia lugha, basi lugha ndiyo nyenzo ya sanaa ya
fasihi, hivyo basi lugha ina dhima muhimu katika ushairi.
USHAIRI WA KISWAHILI KATIKA VIPINDI MBALIMBALI
Katika mjadala huu tutatumia mkabala wa kimapokeo kama alivyojadili N.O.MMBAGA, makabala huu si mgeni
katika kuchambua historia ya ushairi wa Kiswahili.
Ni muhimu kujua kwamba bara la Afrika si bara la giza bali watu
wakeasilimia kubwa ni weusi. Vifuatavyo ni vipindi muhimu sana katika kusoma historia ya ushairi wa
Kiswahili;
- KIPINDI CHA 1884-1913
Katika kipindi hiki mashairi mengi
yaliibuka, wakati huu mashairi yalikuwa ya kiitikadi, itikadi hiyo tunaweza
kugawanya katika mafungu yafuatayo:
a.
ya kati na kisimulizi.mfn, Elmandjebu.
Ya hakiko au ya kishambulizi haya
yilipinga ukoloni, mfn, Buhry.
b. mashairi ya kupinga ukoloni mfano, elkadri
c. mashairi ya vibaraka au walamba
viatu. Mfn sifa za wazungu.
- KIPINDI CHA 1918- 1949
Fasihi ya Kiswahili katika kipindi
hiki cha ukoloni wa kiingereza tunaweza
kuihakiki chini ya fasihi ya kikoloni, ambayo ilijaa vionjo vya kidini, hii
tunaweza kuigawa katika mafungu yafuatayo:
- maadili
- malimwengu
- ya kidini
- tafsiri,
mashairi
mengi ya kipindi hiki yalijitokeza katika gazeti la kikoloni lijulikanalo
Mpangilio huu unafanana kidogo na mpangilio wa Kezilahabi E.
katika makala yake ya Uchunguzi katika Ushairi wa Kiswahili FASIHI, TUKI
(1983).
Kezilahabi E. anagawanya historia ya ushairi wa Kiswahili
katika mihula kama ifuatavyo:
- muhula wa urasimu 1128-1885,
katika muhula huu kezilahabi
anataja tenzi kama vile
ü
utenzi wa Tambuka (1149) (1690)
ü
utenzi wa Al-inkshafi (1810-1820)
ü
utenzi wa Mwana kupona
ü
utenzi wa Ayubu
ü
utenzi wa Ngamia na paa
ü
utenzi wa Masahibu
ü
utenzi wa Kiyama
ü
utenzi wa mikidadi Mayasa
ü
utenzi wa RasL’ Ghuli
ü
utenzi wa Shufaka
ü
mashiri ya Muyaka bin Haji
ü
mashairi ya Bwana Mutaka na Ali Koti
- Muhula wa utasa 1885- 1945
Katika muhula huu zipo pia tenzi kama vile:
ü
Utenzi wa vita vya majimaji
ü
Utenzi wa vita vya uhuru
ü
- Muhula wa urasimi Mpya 1945- 1960
Hapa anawataja washairi kama akina
Shaaban Robert, Amri Abed, Khamis Amani(Nyamaume), Mathias Mnyampala, Ahmed
Nassir, Mdanzi Hanass, Kibwana, Abdi Matunga, M.M Kihere n.k
- muhula wa sasa 1967 hadi leo
hapa ingawa hawataji washairi
mashuhuri wa kipindi hiki nitawataja wachache miongoni mwao akiwemo Kezilahabi
E, M.M. Mulokozi na Kahigi, A. Abdalla n.k
historia ya ushairi wa Kiswahili
ina mikabala mingi basi kama ni hivyo endelea
kufuatilia muhadhara ujao. Nakutakia kazi njema asante kwa kunisikiliza.
Kwa chanzo muhimu cha habari hii
soma – makala za semina ya kimataifa ya waandishi wa Kiswahili III, FASIHI
(2003:148-150)
Tutaendelea.....................
No comments:
Post a Comment